24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

URAIA USIWE KIKWAZO KUWASHIRIKISHA DIASPORA

TANZANIA si nchi masikini kama wengi wanavyoifikiria na mawazo haya yamejengwa toka enzi za ukoloni. Tanganyika ni mkusanyiko wa watu wenye makabila tofauti. Falsafa ya hawa watu waliotawala sehemu hizi ya kuwatenganisha watu kwa kuweza kuwatawala.

Kwanza unachora mpaka halafu unaiita nchi halafu unawatenganisha kuweza kuwatawala. Unachukua lugha yako na kuwalazimisha kuacha lugha zao na kufanya wapuuze tamaduni zao na kuchukua mila na desturi za kutoka kwenu. Ukishawafanya kuwa nchi unaanza kwa ujumla kuchukua nguvu zao kwa kujenga kwako.

Katika kuweka mipaka imetutenganisha diaspora wasiweze kutumia nafasi yao kutengeneza kwenye nchi mama. Hizi ni rasilimali kubwa ambazo zinatoka kule diaspora waliopo kwenda kule walipozaliwa.

Sheria na mfumo uliopo unaleta uzuiaji kwa jamii hiyo ya nje kushiriki kikamilifu. Ni rasilimali ngapi zinazotoka Tanzania kupitia ‘wawekezaji’ wa nje kupelekwa kwenye mabenki yao. Diaspora wanataka kubadilisha hilo na kurudisha hiyo nguvu ya kiujuzi na fedha kuwekeza kwenye nchi-mama.

Watanzania wanaoishi nje ya nchi yao wananyimwa haki zao za kihalisi kwa sababu si tena raia wa hiyo nchi ambayo ina mipaka ya kuchorwa na wakoloni, hawana tena lile karatasi linalosema wao wanaishi hapo kwa hiyo wamepoteza haki zao.

Hapa inaonyesha wazi kwamba wanaadhibiwa na wanaonekana kama wasaliti kwa sababu si tena raia wa nchi hiyo. Binafsi nimeliangalia hili suala nikaona kweli kunahitajika mtazamo mpya. Wasipotambuliwa kama wazaliwa, Tanzania itapoteza rasilimali muhimu sana.

Diaspora itaweza kusaidia sana kazi kwa ajili ya ujenzi na uendelezi wa nchi-mama zinazoendelea. Hivyo inawezekana tu kama hizo nchi mama zitawakubali na kuwapa hiyo nafasi na fursa ya kushiriki katika maendeleo ya nchi mama.

Mpaka sasa juhudi kubwa sana ya wana diaspora imekuwa zaidi katika ngazi ya mtu binafsi na jamii ambayo anatoka na umakini na kulenga zaidi katika mahusiano wa mtazamo ‘nini naweza kufanya kwa jamii yangu’ kazi nyingi imefanyika katika ngazi za chini.

Ni jambo la utaratibu ambao halileti tija kwa nchi kuwazuia waliozaliwa nchini na ambao wanaishi nje kutokushiriki katika uzalishaji nchini Tanzania. Ukiwachukulia hawa kama wawekezaji wengine kutoka nje ni kuinyima nchi fursa ambazo zitawasaidia wengi nje na ndani ya nchi.

Hii ina maana kwamba mipango mingi ya wanadiaspora imefanyika kimtu binafsi na kazi imefanyika kwa misingi ya kusaidia ndugu na jamaa. Na bila shaka, hii ina athari chanya kitaifa si moja kwa moja. Hali ya ndugu na jamaa huwa ni nzuri.

Mfumo huu si mbaya lakini utaweza kuzidisha sana mapato ya nchi na kuongeza ajira kama hawa wana diaspora wanasaidiwa kimfumo kuweza kuwekeza bila vikwazo na masuala ambayo yanasaidia katika maendeleo.

Kupitia uwezo wa kuitisha mkusanyiko na kutengeneza mitandao kimataifa, diaspora na mitandao yao na uwezo wao asili kwa ajili ya ukuaji wa kiujuzi na maendeleo, katika ngazi mbalimbali nchini, wataalamu na ngazi hata za kimataifa, kundi hili la watu wanaweza kutafuta fedha na misaada ya kimataifa kwa shughuli nyingi au miradi Tanzania.

Mara nyingi wakati Tanzania inaonyesha bidhaa zake nje na sehemu za uwekezaji diaspora wanaweza kusaidia sana. Katika mfumo huu Tanzania itaongeza utalii na kuwawezesha wananchi wake wakaweza kupata mwamko na shauku ya kujitegemea zaidi na kushirikiana kiujasiriamali na waliokuwa nje ya nchi.

Diaspora ni rasilimali ya pamoja ya Tanzania na Watanzania zilizopo nje ya mipaka yake. mtaji huu wa binadamu kama ukitumika vizuri kwa ufanisi na kimaarifa, itawapatia Tanzania msingi wa maarifa kwamba unaweza kutumia ili kupata habari na utaalamu ili kusaidia kupunguza makali ya mabadiliko makali ya kugeuza mwenendo na upindo wa mwelekeo na kuepuka kupiga kuta za matofali. Hii inapaswa kuonekana kama chanzo nyongeza ya rasilimali za kitaifa zilizopo.

Kuimarisha diaspora na mfumo ambao husaidia ushirikiano wa kundi hilo na ushiriki katika maendeleo ya nchi itasaidia wazi na kusafisha njia kwa ajili ya Tanzania, hii itasaidia kwa kiasi kikubwa ushirikiano wa nchi katika uchumi wa dunia.

Hii itakuwa pia kufungua mazungumzo mbalimbali na viwango tofauti kati ya waliopo nje ya nchi na ndugu zao jamii ya Tanzania na kujenga umoja ambao utakuwa athari chanya juu katika mchakato wa maendeleo ya nchi.

Moja ya mbinu ya wanadiaspora ni kuwafikia wote kwenye nchi-mama na kufanya kazi kwa pamoja na kuelewa mahitaji ya nchi.

Ukishafahamu haya yote, basi iliyobaki ni kasi tu ya kutekeleza uliyoyalenga.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles