27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

UPINZANI NIGERIA WASEMA BUHARI HAFAI KUONGOZA                    

ABUJA, NIGERIA


CHAMA kikuu cha upinzani nchini Nigeria, Peoples Democratic (PDP) kimesema Rais Muhammadu Buhari hafai kuiongoza nchi hiyo baada ya kusafiri tena kwenda London, Uingereza kwa matibabu.

Buhari (75) alikaa miezi mitano jijini London akitibiwa ugonjwa, ambao haukuwekwa wazi, lakini aliokuwa akiongezewa damu mwilini mara kadhaa.

Aliondoka tena mapema wiki hii, akisema safari hiyo ilitokana na ombi la daktari wake, na kuahidi kurudi Nigeria Jumamosi.

Lakini PDP kimesema katika taarifa yake kuwa ziara hiyo inaonyesha Buhari hayupo sawa kiafya na hivyo hafai kuongoza Taifa.

Kabla ya uchaguzi wa 2015, chama cha PDP, ambacho wakati huo kilikuwa madarakani, kilidai Buhari alikuwa na saratani ya kibofu.

Buhari alikanusha madai hayo akisema ripoti ya matibabu iliyofichuliwa ikionyesha anatibiwa hali hiyo, ilikuwa ya uongo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles