33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Uongozi wa juu wa Chadema wakamatwa

washukiwa

Viongozi wa Chadema zaidi ya 60 wakiwemo wabunge na viongozi wa kitaifa, mwenyekiti, katibu mkuu, makamu mwenyekiti, naibu bara, naibu zanzibar wamekamatwa leo na jeshi la polisi likiongozwa na OCD wa Oysterbay majira ya saa 9 wakiwa katika kikao cha pamoja cha kamati kuu kilichokuwa kikifanya katika Hoteli ya Giraffe.

Viongozi hao walifikishwa wa katika Kituo Kikuu cha Polisi Kati (Central) kwa mahojiano zaidi.

Akizungumzia hatua ya kukamatwa kwa viongozi hao, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (Chadema), alisema wameshangazwa na hatua hiyo ambayo aliita ya uonevu.

Alisema hatua ya kukamatwa kwa viongozi wa Chadema si jambo la kushangaza kwani pamoja na hali bado hawajakata tama na wataendelea na harakati za kudai demokrasi ya kweli nchini.

Aliongeza kuwa kikao hicho kulikuwa na wajumbe 178.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles