31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Ummy: Tunaendelea kutekeleza mpango wa kudhibiti wadudu dhurifu

Amina Omari – Tanga

Serikali imesema itaendelea kutekeleza Mpango kabambe wa Taifa wa kudhibiti Mbu na wadudu dhurifu nchini ili kudhibiti magonjwa kama malaria, Dengue, homa ya manjano, matende na mabusha kwa kununua madawa na vifaa vya kupulizia dawa za kuua mbu pamoja wadudu wanaozambaza magonjwa hayo.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, wakati wa Uzinduzi wa uhamasishaji wa mkakati wa udhibiti wa mbu na wadudu dhurifu katika Halimashauri ya Jiji la Tanga.

Amesema kuwa ili kuimarisha kampeni ya kutokomeza mbu nchini, Wizara imeipatia Halmashauri ya Jiji la Tanga mashine kubwa ya kisasa (Fogging Machine) ya kupuliza dawa ili kuuwa mbu wapevu na wadudu dhurifu.

Aidha Waziri Ummy amesema kuwa Wizara itaendelea kubuni mikakati mingine zaidi na kutafuta rasilimali fedha ili kutokomeza mbu na wadudu dhurifu nchini.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles