27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Ulinzi mkali Netanyahu akiwasili Rwanda

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kushoto na Rais wa Rwanda Paul Kagame.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kushoto na Rais wa Rwanda Paul Kagame.

KIGALI, RWANDA

ULINZI mkali ulishuhudiwa jana katika mji mzima wa Kigali wakati Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu akiwasili kwa ziara ya siku moja.

Wakati askari wakiwa wametanda kila kona ya jiji, barabara kuu zinazounganisha mji huo mkuu na uwanja wa ndege zilifungwa na kusababisha foleni na usumbufu mkubwa.

Netanyahu aliye ziara ya siku nne barani Afrika yuko hapa kwa saa chache ambapo pamoja na mambo mengine atatembelea kumbukumbu ya mauaji ya kimbari huko Gisozi na anatarajia kufanya mazungumzo na Rais Paul Kagame katika Kijiji cha Urugwiro.

Wakati akiwasili alikaribishwa na Kagame na kukagua gwaride la heshima uwanja wa ndege kabla ya kuelekea Gisozi anbako kuna mabaki ya mauaji ya kimbari ya mwaka 1994.

Wawili hao walitarajia kufanya mkutano wa pamoja na wahabari kabla ya Netanyahu kuhitimisha ziara yake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles