30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

UINGEREZA YAKASIRISHWA MAREKANI KUVUJISHA SIRI

LONDON, UINGEREZA


POLISI wa Uingereza wamesitisha kubadilishana taarifa za siri na Marekani zinazohusu shambulio la bomu la kujitoa mhanga mjini Manchester.

Hatua hiyo imeripotiwa kuwa inatokana na hofu ya kuvuja kwa  taarifa hizo katika vyombo vya habari nchini Marekani, hali inayoweza kuvuruga msako wa mtu anayeaminika kuhusika katika utengenezaji wa bomu lililoua watu 22, Jumatatu wiki hii.

Iwapo itathibitishwa, hatua  hiyo  ya  kuzuia  kupeana  taarifa  na mshirika wake muhimu  kabisa  katika  ulinzi na  usalama, itaonyesha kiwango cha  hasira ya  Uingereza kuhusu vitendo vya uvujishaji siri kwa vyombo vya habari vinavyoshuhudiwa nchini Marekani sasa.

Waziri  Mkuu  wa  Uingereza,  Theresa  May,  alitarajia kuzungumzia hilo wakati wa  mkutano wake  na  Rais  Donald Trump wa  Marekani  mjini Brussels, Ubelgiji jana.

Hilo linakuja baada ya gazeti  la  New York Times  kuchapisha  picha za  eneo  lililotokea  mashambulizi  mjini  humo, nyaraka ambazo walibadilishana na wenzao wa Marekani.

Shambulio hilo lilitokea Jumatatu wiki hii katika ukumbi  wa  tamasha  la  muziki  uliojaa  watu  kaskazini  mwa mji huo.

Picha  hizo  ni  pamoja  na  mabaki  ya  bomu  linaloshukiwa kutumiwa katika  shambulio  hilo, mfuko  wa  kubeba  mgongoni uliokuwa  umebebwa  na  mshambuliaji  wa  kujitoa  mhanga na kuonyesha  damu  katika mabaki  ya  magari  yaliyoharibiwa.

Katika siku za hivi karibuni, Rais Trump mwenyewe na maofisa wake wamekuwa wakishutumiwa kuvujisha kwa vyombo vya habari na Urusi taarifa za kijasusi inazopewa na washirika wake.

Baada  ya  shambulio  baya  kabisa  kuwahi kutokea Uingereza   tangu mashambulizi ya kigaidi ya mwaka  2005, polisi  iko katika  msako kumtafuta  mshirika  inayemshuku alimsaidia  Salman Abeid kutengeneza  bomu  hilo.

Kwa mujibu wa taarifa za kijasusi za Ujerumani, raia huyo wa Uingereza mwenye asili ya Libya, alizuru mji wa Dusseldorf, Ujerumani siku  nne  kabla  ya kuendesha shambulio  hilo la kujitoa mhanga. 

Mji huo ulio kilometa  300 magharibi mwa  mji  mkuu  wa Berlin, unaelezwa kuwa na wahamiaji wengi kutoka mataifa ya Kiarabu hasa wenye itikadi kali za kidini.

Wachunguzi  wanaonyesha   Abedi alikuwa  sehemu  ya  mtandao mpana  wa  wanamgambo wanaoendesha harakati za kigaidi.

Kinachowapa  hofu  majirani wa Abedi  hivi  sasa  ni uhusiano  ambao  haujulikani  kati  yake na  ndugu  zake ambao ni  washukiwa  na  kati ya shambulio  hilo  na  imani  yake. 

Wakati  baba  yake  Abedi  na ndugu  zake  wanashikiliwa  kwa  uchunguzi  nchini Libya, wanahabari wamezuru msikiti  mkubwa  mjini  Manchester kutaka  kujua ushahidi  wa  kuhusika katika  shambulio  hilo. 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles