30.2 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Uingereza, Marekani kususia mkutano Saudi Arabia

LONDON,England

UINGEREZA na Marekani zinatafakari kususa mkutano mkubwa wa mataifa unaotarajiwa kufanyika  Saudi Arabia.

Ni kutokana na  kitendo cha kupotea mwandishi wa habari,  Jamal Khashoggi,akiwa katika ubalozi wa nchi hiyo  mjini Istanbul,  Uturuki.

Khashoggi, ambaye alikuwa   mkosoaji mkubwa wa Serikali ya  Saudi Arabia, alitoweka tangu Oktoba 2 mwaka huu baada ya kuingia ndani ya ubalozi huo.

Uturuki inaamini kwamba mwandishu huyo aliuawa na makachero wa Saudi Arabia, madai ambayo yanakanushwa na nchi hiyo.

Wakati nchi hizo zikizidi kuvutana, Rais wa Marekani, Donald Trump amekwisha kutangaza kuiadhibu Saudi Arabia endapo ikibainika inahusika.

Pia wafadhili na vyombo vya habari wameshajitoa kuudhamini mkutano huo ambao utafanyika baadaye mwezi huu mjini Riyadh,  kwa kile wanachodai ni kuwa na wasiwasi na   maisha ya  Khashoggi.

Wanadiplomasia  walimweleza Mwandishi wa   BBC, James Landale kwamba mawaziri wote wawili wa fedha, Steve Mnuchin wa Marekani na   Uingereza, Liam Fox  huenda wasihudhurie tukio hilo ambalo limeandaliwa na Mwana wa Mfalme, Mohamed bin Salman  kuhamasisha ajenda zake mpya.

Msemaji wa Idara ya Biashara ya Uingereza, alisema  ratiba ya Dk.  Fox  bado hajakamilika kwa ajili ya kuhudhuria mkutano huo wa wiki moja.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles