26.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Uganda na DRC yazindua mradi wa barabara

Kasese, Uganda

Rais wa Uganda Yoweri Museveni na Rais wa Jamahuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi wamezindua mradi wa ujenzi wa barabara kati ya nchi hizo mbili.

Hafla ya uzindunzi wa mradi huo ulifanyika katika mji wa mpakani wa Mpondwe wilaya ya Kasese magharibi mwa Uganda na Kasindi katika mkoa wa Kivu kaskazini mwa DRC.

Katika taarifa ya pamoja viongozi hao wawili mradi huo utaimarisha uchumi na maisha ya raia wao.

Walisistiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiana katika masuala ya usalama, biashara, uwekezaji na usimamizi wa maji ya mpakani, mafuta ya petroli na madini.

Mwezi Mei mwaka huu, nchi hizo mbili zilitia saini mikataba mitatu ya ujenzi wa barabara ya umbali wa kilo mita 223 sawa na (maili 138).

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles