Kigali, Rwanda
Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema nchi yake ilikuwa na jukumu la kisiasa katika mauaji ya kimbari ya Rwanda na kuwaomba manusura “kuwasamehe” wakati wa ziara yake mjini Kigali leo.
Katua hiyo ilitarajiwa katika hotuba yake katika ukumbi wa makumbusho ya mauaji ya kimbari mjini Kigali, jambo ambalo halikufanywa na watangulizi wake katika kipindi cha miaka 27.
Macron amekiri jukumu la Ufaransa ni “deni kwa wahasiriwa baada ya kimya cha muda mrefu”.
“Kwa kufanya hivyo, wale walionusurika usiku huo, huenda pengine wakatusamehe, (na) kutupatia zawadi ya msamaha,” amesema Macron.
Rais wa Ufaransa ameahidi enzi mpya na kumalizika kwa ‘miaka 27 ya utengano, kutokuelewana na mateso’.