31.2 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Ubunge 2020 mwiba kwa wateule wa JPM

Na EVANS MAGEGE – Dar es Salaam

MAANDALIZI ya kutafuta majimbo ya kugombea ubunge katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 yanaonekana kupata kikwazo kwa baadhi ya viongozi wa Serikali.

Hali hiyo inatokana na onyo lililotolewa hivi karibuni na Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, aliyewataka viongozi hao kuacha mara moja mikakati hiyo wakati bado ni watumishi wa umma na aliwashauri waridhike na nafasi walizoteuliwa na Rais Dk. John Magufuli.

Viongozi walionyoshewa kidole na Dk. Bashiru ni wakuu wa mikoa, makatibu tawala wa mikoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri na wakuu wa mashirika ya umma walioanza kujipitisha katika baadhi ya majimbo kimkakati, kuendesha kampeni za chinichini kutafuta uungwaji mkono wa kugombea ubunge.

Akizungumza wiki iliyopita na wananchi wa Kijiji cha Lagangabilili kilichopo Itilima mkoani Simiyu, Dk. Bashiru alisema viongozi wengine wameanza kutembea na wagombea wanaowataka na kuanza kuwapigia kampeni za chinichini.

Onyo hilo, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa wanatalitafsiri kama mbinyo wa kinidhamu utakaowashughulikia viongozi wenye tabia za …

Kwa habari zaidi jipatie nakala yako ya MTANZANIA.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles