25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

TWAWEZA YATAKIWA KUJIELEZA KUFANYA UTAFITI BILA KIBALI

Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Siku chache baada ya kutoa utafiti wake, Taasisi isiyo ya Serikali ya Twaweza imeandikiwa barua na Tume ya Sayansi na Teknolojia (Costech) ikitakiwa kujieleza ndani ya siku saba ni kwa nini isichukuliwe hatua za kisheria kwa kufanya na kutoa matokeo ya utafiti kuhusu maoni ya wananchi bila kibali.

Kwa mujibu wa barua hiyo inayodaiwa kuandikwa na Mkurugenzi wa Costech, Amos Nungu imesema Twaweza waliwasilisha maombi ya vibali vya kufanya utafiti wa awali nchini lakini utafiti huo wa Sauti ya Wananchi haukuwasilishwa katika maombi yao.

Soma zaidi… http://mtanzania.co.tz/wameporomoka/

“Matokeo ya utafiti huo yanakiuka kifungu cha 11 cha Mwongozo wa Kusajiliwa na Kuidhinishwa kwa Usajili wa Kitaifa kwa kutoandikisha mradi huu wa utafiti kwa Costech,” imesema sehemu ya barua hiyo.

Katika utafiti huo wa Twaweza, matokeo yalionyesha kuporomoka kwa umaarufu wa rais, vyama vya siasa, wabunge na madiwani.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles