23.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

TWAWEZA: HALI YA CHAKULA NCHINI NI MBAYA

 

NA ELIZABETH HOMBO

DAR ES SALAAM

NUSU ya kaya za Tanzania sawa na asilimia 69 zinahofia kuishiwa chakula huku asilimia 51 ya kaya hizo zimeripoti kwamba hakukuwa na chakula cha kutosha kulisha kaya nzima.

Matokeo hayo yametolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze ambapo pamoja na mambo mengine asilimia 84 ya wananchi wanaoishi vijijini, wameripoti uhaba wa chakula katika maeneo wanayoishi ikilinganishwa na wale wanaoishi maeneo ya mijini ambapo asilimia 64 wameripoti tatizo hilo.

“Asilimia 51 ya kaya zimeripoti kutokuwa na chakula cha kulisha kaya nzima au mwanakaya kushinda na njaa kwa sababu hakuweza kupata chakula huku asilimia 78 ya wananchi waliohojiwa wameripoti hali ni mbaya katika maeneo wanayoishi.

Matokeo hayo yaliyotolewa na Twaweza katika muhtasari uitwao Uchungu wa Njaa, umetokana na takwimu za Sauti za Wananchi ambao ni utafiti wa kwanza barani Afrika unaotumia njia ya simu.

Takwimu za muhtasari huo wa ripoti kuhusu upungufu wa chakula, zimekusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,800 wa Tanzania Bara.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles