25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Tundaman: Nipo tayari kuwasaidia vijana wa Manzese

TUNDA MANNA JENNIFER ULLEMBO
MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Khalid Ramadhan ‘Tundaman’, ameweka wazi kwamba yupo tayari kutoa msaada kwa vijana wanaoishi maeneo ya Manzese jijini Dar es Salaam.
Akifafanua kauli yake hiyo, alisema anatamani awe daraja la mafanikio kwa vijana hasa waliokata tamaa ya maisha ili awaongoze katika maisha mapya na ya matumaini.
“Nipo tayari kuwasaidia hata katika ushauri hasa vijana waliokata tamaa ya maisha wasisite waje nyumbani hata kama sitakuwepo, watakutana na wazazi wangu watawaelekeza nilipo maana nikifanya hivyo itasaidia sana kubadilisha fikra za vijana wengi wanaokimbilia kwenye dawa za kulevya, unywaji wa pombe na uvutaji wa bangi,” alisema Tundaman.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles