27.1 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Tshishimbi kutua AS Vita

NA ZAINAB IDDY-DAR ES SALAAM

ALIYEKUWA nahodha wa Yanga, Papy Tshishimbi,ameweka wazi kuwa kama mambo yatakwenda vizuri atajiunga na Klabu ya AS Vita ya nchini kwao Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC).

Tshishimbi aliondoka jijini Dar es Salaam juzi kurejea DRC,akiwa na mshambuliaji David Molinga.

Tshishimbi na Molinga walipewa mkono wa kwaheri na Yanga,baada ya mikataba yao kumalizika msimu uliopita wa Ligi Kuu Tanzania Bara ulipofika tamati.

Tshishimbi ambaye ni kiungo alishindwa  kuafikiana kwenye maslahi,wakati Molinga
alitemwa kutokana na kutokidhi matarajio dimbani. 

Akizungumza na TANZANIA kabla ya kutimkia DRC, Tshishimbi alisema kuwa wakala wake ameanza mazungumzo na AS Vita, ambayo imeonyesha nia ya kumsajili.

“Wakala wangu ameniambia kuna timu mbili zinanihitaji kule nyumbani mojawapo ni AS Vita, sijaona kama ni tatizo nitaenda kufanya kazi huko kama mazungumzo yatakwenda vizuri.

“Nawashukuru Watanzania hususani mashabiki wangu wa Yanga walioonyesha mapenzi kwangu naahaidi kuwaheshimu na kuwapenda siku zote, kwa sababu nina uhakika ipo siku nitarudi tena Tanzania kufanya kazi,”alisema Tshishimbi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles