24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Trump: Hillary achunguzwe matumizi ya dawa kabla ya mdahalo

clinton_trump_split

WASHINGTON: MAREKANI

MGOMBEA wa urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican, Donald Trump, amemshutumu mpinzani wake wa Chama cha Democrat, Hillary Clinton kuwa huenda alitumia aina fulani ya dawa, wakati wa mjadala wao uliopita.

Alisema  alikuwa na haiba mwanzoni mwa mjadala huo.

Trump alipendekeza  wote wafanyiwe uchunguzi wa matumizi ya dawa kabla ya kufanyika   mjadala wao wa mwisho   Jumatano  wiki hii.

Katika mkutano wake wa hadhara  uliofanyika New Hampshire, Trump kwa mara nyingine, alidai kuna njama za kumwibia kura.

Timu ya kampeni ya Hillary, ilisema  wapiga kura sasa wameona bayana kile anachokiita juhudi za aibu za Trump za kutaka kuhujumu shughuli za upigaji kura.

Umaarufu wa Trump umezidi kudidimia katika majimbo mengi, huku akikabiliwa na madai ya kudhalilisha wanawake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles