28.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Trump aitupia lawama Democratic kushindwa kwa mkutano wake na Kim

WASHINGTON, MAREKANI

RAIS Donald Trump amewatupia lawama wakosoaji wake wa Chama cha Democratic kuwa wamesababisha kushindikana kwa makubaliano baina yake na Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong un.

Trump aliondoka kwenye mkutano huo nchini Vietnam bila ya kufikia makubaliano yoyote na Kim wiki iliyopita baada ya kutofautiana kuhusu masharti ya kuondoa vikwazo ilivyowekewa Korea Kaskazini.

Kupitia ujumbe aliouandika kwenye ukurasa wake wa Twitter Jumapili usiku, Trump aliwakosoa wana-Democrats kwa kuandaa kikao cha Bunge na wakili wake wa zamani, Michael Cohen wakati ambao alikuwa kwenye mazungumzo nyeti nje ya nchi.

Katika ujumbe huo, Trump aliandika kuwa wana-Democrats wameamua kumhoji mtuhumiwa mwongo na mdanganyifu wakati kuna mkutano muhimu wa nyuklia na Korea Kaskazini.

 “Huu ni mtindo mpya dhaifu katika siasa za Marekani na pengine ndio chanzo kilichofanya mkutano huo kutofanikiwa,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles