24.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Trump aitaka Ulaya kuwapokea wapiganaji wa IS

WASHINGTON, MAREKANI

RAIS wa Marekani Donald Trump juzi aliyataka mataifa ya Ulaya yachukue mamia ya wapiganaji wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu (IS) nchini Syria, akitishia kuwa bila hivyo Marekani italazimika kuwaachia huru.

“Marekani  inazitaka  Uingereza, Ufaransa, Ujerumani  na  mataifa mengine washirika wa  Ulaya kuwachukua zaidi ya wapiganaji 800  ambao wamekamatwa Syria na  kuwafikisha mahakamani,” rais  huyo  aliandika  katika  mfululizo wa maandishi yake kwenye akaunti yake ya Twitter.

“Eneo la  Ukhalifa linakaribia kuanguka. Mbadala  wake  si  mzuri  kwa sababu  tutalazimika kuwaachia  huru. Marekani  haitaki  kuwa  walinzi  wa  wapiganaji hawa wa ISIS kutoka Ulaya, ambako  ndiko wanatarajiwa  kwenda.

“Tunafanya  mengi na tunatumia  fedha  nyingi, sasa  wakati  umefika wengine  kuchukua   jukumu  hilo na  kufanya  kazi, ambayo wanaweza  kuifanya.”

“Tunaondoa  majeshi  yetu  baada  ya ushindi  wa  asilimia  100  dhidi  ya IS!”

Trump  alisababisha  wasi wasi  mkubwa  Desemba  mwaka jana wakati alipotangaza ghafla kuwa Marekani  itaondoa askari wake kutoka Syria na kwamba  IS tayari limeshindwa.

Wakosoaji walionya kundi hilo halijashindwa wala kutokomezwa na kujiondoa  kwa  Marekani  kunaweza kulifufua kwa vile washirika  wa Marekani waliopo eneo  hilo hawana  uwezo wa kupambana na kitisho  hicho  peke  yao.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles