26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Trump achunguzwa kutaka kuiuzia Saudia nyuklia

WASHINGTON, MAREKANI

WABUNGE wa Marekani wamesema wanafanya uchuguzi iwapo Rais Donald Trump anajaribu kuuza teknolojia nyeti ya nyuklia kwa Saudi Arabia, ili kuwafurahisha wafuasi wake wafanyabiashara, ambao watafaidika na mpango huo.

Bunge la Marekani tayari limeshafungua uchunguzi dhidi ya pendekezo la utawala wa Trump, la kutaka kujenga vituo kadhaa vya nyuklia nchini humo. Mbunge Elijah Cummings, Mwenyekiti wa Kamati ya Halmashauri ya Uangalizi na Mageuzi, ameitaka Ikulu ya Marekani kuwasilisha nyaraka za suala hilo.

Inasemekana kuwa kuna mkutano uliofanyika miezi miwili tu baada ya Trump kuingia madarakani kati ya mkwewe, Jared Kushner, na mwanamfalme Mohammed bin Salman wa Saudi Arabia , muda mchache kabla ya kutangazwa kuwa mrithi wa kiti cha ufalme wa taifa hilo.

Ripoti ya Kamati ya Uangalizi ya Baraza la Wawakilishi imesema mshauri wa zamani wa usalama wa taifa Michael Flynn na wenzake wawili ndio waliopendekeza mpango huo.

Waliuwasilisha kwa Tom Barrack, mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Sherehe ya kuapishwa kwa rais, na muungano wa kampuni za Marekani yakiongozwa na makamanda wa kijeshi waliostaafu na viongozi wa zamani wa Ikulu ya Marekani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles