22.8 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Trilioni mbili zatumika miradi ya kimkakati majiji sita

Amina Omari, Tanga

Serikali imetumia zaidi ya Sh trilioni mbili kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kimkakati katika majiji sita nchini.

Hayo yamebainishwa na Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi, Selemani Jaffo wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotelezwa na Halmashauri ya Jiji la Tanga.

Amesema kuwa miradi hiyo ina lengo la kuleta taswira mpya za kimaendeleo ikiwemo muonekano tofauti katika majiji hayo .

“Tumejenga barabara kwa kiwango cha lami na kuweka taa za barabarani, ujenzi wa madampo ya kisasa pamoja na maeneo ya kisasa ya biashara hiyo ni baadhi ya miradi ambayo inaendelea katika majiji hayo”amesema Jaffo.

Hata hivyo amewataka wakuu wa mikoa walioko katika majiji hayo kuhakikisha wanasimamia kwa ukaribu miradi hiyo iweze kuwa ni yenye viwango vyenye ubora na inayozingatia thamani halisi ya fedha.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles