25.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Tiwa Savage awajia juu wasanii Nigeria

TiwaLAGOS, NIGERIA

NYOTA wa muziki nchini Nigeria, Tiwa Savage, amewataka wasanii wa kiume nchini humo kuachana na tabia ya kuomba rushwa ya ngono kwa ajili ya kuwasaidia wasanii wachanga.

Mrembo huyo amedai kwamba kuna baadhi ya wasanii ambao wana tabia ya kutaka kuwasaidia wasanii wa kike ambao ni wachanga kwenye muziki lakini kwa kuwataka watoe rushwa ya ngono ili wawasaidie.

“Kuna wasichana wengi katika tasnia ya muziki kwa sasa na wapo ambao wanatamani kufika hapo ila kuna changamoto kubwa sana hasa pale wanapoomba kufanya kazi na wasanii wa kiume ambao wana majina makubwa.

“Wengi wao wanaombwa kutoa rushwa ya ngono kwa ajili ya kuwasaidia, hivyo wanatakiwa kuwa makini na wasanii hao kwa kuwa wanaweza kuwaharibia mipango ya maisha yao, hata mimi nimepitia huko lakini uwezo wangu ukanifanya niwe hapa nilipo kwa sasa bila misaada yao,” alisema Tiwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles