31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Tiwa Savage ajutIa ndoa yake

Tiwa SavageLAGOS, NIGERIA

NYOTA wa muziki nchini Nigeria, Tiwa Savage, amedai kuwa anajuta kuweka wazi mambo yake ya ndoa katika mitandao ya kijamii.

Msanii huyo kwa sasa kazi zake zinasimamiwa na kampuni ya Rock Nation, inayomilikiwa na mkali wa rap nchini Marekani, Jay Z.

Tiwa amedai kuwa kwa siku za hivi karibuni amekuwa akiyaweka mambo yake ya ndoa katika mitandao, hasa baada ya kuhojiwa mara kwa mara, lakini kitendo hicho kimewafanya watu wamzungumzie vibaya.

“Katika kitu ambacho naweza kusema kuwa nimekosea katika maisha yangu ni kuweka wazi mambo yangu ya ndoa, najuta kwa kuwa kuna watu ambao wananiongelea vibaya kutokana na taarifa ambazo niliziongea, kuanzia sasa siwezi kufanya hivyo tena kwa mambo yangu binafsi,” amesema Tiwa

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles