27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 16, 2024

Contact us: [email protected]

Tiger Wood ashinda taji la 15 baada ya miaka 11

GEORGIA, MAREKANI

NGULI wa mchezo wa golfu  duniani, Tiger Woods, ameshinda taji la 15  kwenye michuano mikubwa baada ya juzi kutwaa ubingwa  wa  michuano ya Masters iliyokuwa ikifanyika katika Mji wa Augusta Marekani.

Mchezo huo ambao ulichezwa katika Mji wa Georgia, ulimfanya Wood kumaliza ukame wa mataji baada ya miaka 11 akimgaragaza mpinzani wake, Francesco Molinari.

Mara ya mwisho Wood kutwaa taji katika michuano mikubwa ilikuwa mwaka 2005.

Wood (43) alitangaza kustaafu kucheza mchezo huo lakini mwaka 2017, alibadilisha uamuzi wake na kuendelea na mchezo huo.

Nyota huyo tangu ashinde taji la kwanza, imepita miaka 22.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles