25 C
Dar es Salaam
Wednesday, April 24, 2024

Contact us: [email protected]

Tibaijuka afunguka kukataa fedha za UN

MBUNGE wa   Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka (CCM).
MBUNGE wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka (CCM).

Na Editha Karlo

MBUNGE wa   Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka (CCM) amewaeleza wapiga kura wake sababu ya kukataa   tuzo ya Umoja wa Mataifa (UN) ya mamilioni ya fedha kuwa sheria za nchi haziruhusu kiongozi kupokea zawadi.

Profesa Tibaijuka aliyasema juzi kwenye mkutano  wa hadhara na wapiga kura wale  uliofanyika   kwenye Viwanja vya Red Cross Muleba.

Alisema tuzo hiyo ya heshima ambayo hutolewa kila baada ya miaka miwili  na  UN ilikuwa ni kwa ajili ya kuthamini mchango wa kazi alizozifanya.

Mbunge huyo alisema   kukataa fedha hizo ni kukwepa mtego  kama wa  mwaka juzi katka suala la Tegeta  Escrow  ambako alipata mgao wa Sh  bilioni 1.6 kutoka kwa mfanyabiashara wa Kampuni ya VIP.

“Mimi nina marafiki wengi   ndani ya nchi na hata nje ya nchi ambao wanapenda kazi zangu ninazofanya na wapo tayari kunichangia.

“Hizo fedha za tuzo wanazosema nimezikataa hazina tofauti na hela za Rugemalira tena zile ni mbaya zaidi,” alisema Profesa Tibaijuka.

Alisema tuzo hiyo ilikuwa na vipengele vitatu ambavyo ni cheti, kikombe na    dola 100,000 za Marekani (zaidi ya Sh  milioni 200)

.Alisema alikataa  kuzipokea  kwa sababu   ya sheria za nchi zilivyo sasa kwa viongozi  hawaruhusiwi kupokea zawadi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles