27.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

The Rock, Vin Diesel wamaliza ‘bifu’ lao

NEW YORK, MAREKANI

STAA wa filamu nchini Marekani Dwanye Johnson maarufu kwa jina la The Rock, ameweka wazi kuwa kwa sasa hana mgogoro na rafiki yake Vin Diesel.

Msanii huyo ametumia ukurasa wake wa Instagram na kuwashukuru mashabiki zake ambao walikuwa wanataka bifu hilo limalizike ili waendelee na kazi zao kama ilivyo kwenye filamu ya Fast & Furious.

“Napenda kutumia nafasi hii kwa ajili ya kuwashukuru mashabiki wote ambao walikuwa wanataka tuweke pembeni tofauti zetu, kutoka kwa mashabiki jambo hilo limefanikiwa na sasa hakuna tofauti kati yetu, urafiki kama kawaida.

“Namshukuru Vin Diesel kwa sapoti yake kwa kuwa yeye ndiye aliyenifanya niwe kwenye familia ya Fast & Furious, yeye ni kama kaka yangu acha maisha yaendelee,” alisema The Rock.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles