31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

TFDA YANASA MAFUTA YENYE KEMIKALI ZA SUMU

Mwandishi Wetu, Mwanza

Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Kanda ya Ziwa imekamata shehena ya malighafi ya mafuta ya kupikia aina ya Poa Cooking, yanayodaiwa kutengenezwa na viambata vya sumu katika kiwanda cha kuchambua pamba na kusindika mafuta cha ICK cha jijini Mwanza.

Inadaiwa mmiliki wa bidhaa hizo, Mfanyabiashara Mtanzania mwenye asili ya Asia, Baweshi Gandecha, alikuwa anauza tofauti na masharti ya uagizaji wake hivyo kutishia usalama wa walaji.

Meneja wa TFDA Kanda ya Ziwa, Moses Mbambe, amesema bidhaa hizo zina madhara makubwa kwenye mfumo wa chakula kwani husababisha matobo kutokana na kuwa na tabia ya kuunguza chakula na mdomo.

“Mafuta haya yana madhara ya kiafya kwa watumiaji kutokana na kutengenezwa kwa kutumia kemikali aina ya ‘Caustic Soda’ ambayo huathiri mfumo wa chakula kwa kuunguza mfumo huo na midomo na kusababisha matokeo kwenye mfumo wa chakula,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles