27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

TAWLA yawafunda wanahabari

Na Brighiter Masaki, Mtanzania Digital

CHAMA Cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA), kimewakutanisha wanahabari na kujadili nafasi zao katika kuonyesha ushiriki wa wanawake katika shughuli za kiuchumi ili kuhakikisha kunakuwa na usawa katika ushiriki wa shughuli za kiuchumi.

Akizungumza katika mafunzo hayo jijini Dar es Salaam, Mwanahabari mkongwe, Edda Sanga amesema kuwa nafasi ya mwanamke na ushiriki wake katika shughuli za kiuchumi ni mkubwa na kuwataka  wahabari kuwafikia na kuzionesha juhudi hizo zinazofanywa kwa  jamii.

“Wanawake wanahitahi fursa, haki, usawa na ustawi na hili linajidhihirisha wazi wanawake wanajihusisha katika shughuli za uzalishaji mali kwa asilimia 90.4 kupitia kilimo hasa cha jembe la mkono na wanakidhi mahitaji ya chakula kwa nchi nzima kwa asilimia 70,” amesema.

Edda amewataka wanahabari kuwaibua wanawake waliopambana na kuleta matokeo chanya katika jamii, Taifa na familia zao kwa ujumla ili kuleta chachu kwa mabinti na kujenga taifa imara lenye haki na usawa hasa wa ushiriki wa shughuli za kiuchumi na biashara.

Katika semina  hiyo mada mbalimbali zilijadiliwa ikiwamo ushiriki wa wanawake kwenye shughuli za kiuchumi na biashara, vikwazo na namna ya kuwafikia wanawake wengi zaidi na kuvumbua jitihada zao zinazoleta matokeo chanya katika jamii.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles