30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Tanzania na Uganda zasaini mikataba ya sekta ya mafuta na gesi

Kampala, Uganda

Tanzania na Uganda zimesaini mikataba katika maeneo matatu muhimu ya kuendeleza sekta ya mafuta na gesi ya Uganda.

Mikataba hiyo imesainiwa jana Aprili 11, 2021 wakati wa ziara ya kwanza ya nje ya nchi ya Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.

Utiaji saini huo umefanyika kati ya Serikali ya Uganda na Kampuni ya Mafuta ghafi ya Afrika Mashariki (EACOP) juu ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Hoima (Uganda) kwenda Tanga (Tanzania).

Makubaliano kati ya mataifa hayo mawili ya Afrika Mashariki yamejikita katika masuala ya hisa, usafirishaji na ushuru.

Mradi huu una manufaa makubwa kwa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ni ujenzi wa bomba la mafuta ghafi wa jumla ya Kilometa 1,443 kutoka magharibi mwa Uganda hadi kwenye bandari ya Tanga katika bahari ya Hindi, Tanga.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles