27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Tamasha la Shukurani lasogezwa mbele

NA BEATRICE KAIZA, Mtanzania Digital

MUANDAAJI wa tamasha la Shukurani, Alex Msama, amesogeza mbele siku ya kufanyika tamasha ambapo itakuwa ni Oktoba 31, mwaka huu kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam.

Awali tamasha hilo lililoandaliwa na Msama Promotion, lilikuwa lifanyike Oktoba 3, 2021 ambapo kutakuwa na wasanii mbalimbali wa nyimbo za injili akiwamo Upendo Nkone.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 31, Msama amesema wamebadilisha tarehe kutokana na sababu mbalimbali.

“Mashabiki wakae tayari, kwani tumejipanga vizuri na wasanii mbalimbali wakubwa wataimba ‘live’,” amesema Msama.

Amesema tamasha hilo kubwa la mziki wa Injili litakwenda sambamba na kuliombea Taifa na kutoa shukrani kwa Mungu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles