25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

Takukuru yamhoji Mkurugenzi TPA

Dar es Salaam, Tanzania

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya nchini, (TAKUKURU) imemkamata Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari wa Tanzania(TPA), Desudedit Kakoko ili kuhojiwa kuhusu tuhuma za ufisadi.

Kukamatwa kwa, Kakoko kunafuatia kusimamishwa kazi Jumapili iliyopita kama ilivyoagizwa na Rais Samia Suluhu, ili kupisha uchunguzi kuhusu udokozi wa fedha za umma zenye thamani ya dola za kimarekani milioni 1.55.

Rais Samia alimwagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Seri9kali (CAG), Dk. Charles Kichere kuchunguza jinsi Sh bilioni 3.6 zilivyoibiwa kwenye Mamlaka ya bandari.

Ofisa wa Mawasiliano wa TAKUKURU, Doreen Kapwani, amesema kuwa ni kweli wanamshikilia Mkurugenzi wa Bandari, Kakoko kwenye Makao Makuu ya taasisi hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles