27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

TAEC: Watanzania njooni Nanenane mjifunze teknolojia ya nyuklia

Mwandishi Wetu, Simiyu

Wananchi wanaoishi mikoa ya Kanda ya Ziwa na mikoa jirani, wametakiwa kuhudhuria kwa wingi kwenye banda lao katika Maonesho ya Wakulima (Nanenane) kitaifa yanayofanyika katika Uwanja wa Nyakibindi, mkoani Simiyu ili kujipatia elimu ya namna ambavyo teknolojia ya nyuklia inavyotumika katika sekta mbali mbali hapa nchini ikiwemo kilimo, mifugo, maji na afya.

Akizungumza katika banda la tume hiyo, Ofisa Mwandamizi wa Utafiti wa TAEC,  Yesaya Sungita amesema wananchi watapata elimu ambayo itawawezesha kupata uelewa juu ya masuala ya matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia na udhibiti wake hapa nchi ili kutoleta madhara kwa wananchi na mazingira.

“TAEC imekuwa ikihakikisha teknolojia ya nyuklia inatumika ipasavyo katika sekta muhimu kama vile maji, mifugo na kilimo.

“Lakini mbali na wananchi kujua kuhusiana na teknolojia hiyo ya nyuklia, pia wataweza kufahamua namna TAEC inavyofanya kazi ya kusimamia na kuthibiti matumizi salama ya mionzi nchini,” amesema Sungita.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles