27.9 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Sri Lanka: Ibada za Kanisa Katoliki zafutwa kwa wiki ya pili

Ibada za Kanisa Katoliki zimefutwa kwa wiki ya pili katika mji mkuu wa Sri Lanka, Colombo. Serikali imeonya juu ya uwezekano wa kutokea mashambulizi zaidi kutoka kwa kundi lenye mafungamano na Kundi linalojiita Dola la Kiislamu IS ambalo limehusishwa na mashambulio ya mabomu wakati wa sikukuu ya Pasaka.

Padri Edmund Tillakaratne, msemaji wa Parokia ya Colombo, amesema Kardinali Malcolm Ranjith amefuta ibada zote za Jumapili katika jimbo hilo kulingana na ripoti za usalama za hivi karibuni.

Waziri mmoja wa Sri Lanka amesema mawaziri wa serikali wanaweza kulengwa katika mashambulizi ya kigaidi. Wakati huo huo Polisi nchini humo jana jioni walichapisha majina na picha za watu tisa wanaotuhumiwa kuhusika na mashambulio ya siku ya Pasaka kwenye makanisa na hoteli za kitalii yaliyosababisha kuuwa watu wapatao 253.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles