24.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Spurs wamtega Kane

London, Uingereza

KATIKA kumshawishi abaki, klabu ya Tottenham iko tayari kumlipa Harry Kane mshahara mpya wa Pauni 330,000 (zaidi ya Sh bil moja za Tanzania) kwa wiki.

Hizo ni jitihada za Tottenham kumzuia Kane anayeonesha kuvutiwa zaidi na mpango wa kwenda Manchester City, licha ya kwamba amebakiza miaka mitatu katika mkataba wake.

Awali, Tottenham walikataa ofa ya Pauni milioni 120 iliyowekwa mezani na Man City, wakisisitiza wanataka Pauni milioni 150.

Wakati huo huo, bado zipo taarifa zinazodai Kane mwenye umri wa miaka 28 hana raha kuona Mwenyekiti wa Tottenham, Daniel Levy, anazuia asiende Etihad.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles