30.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Somalia yapokea chanjo ya Covid 19

Mogadishu 

Waziri wa afya nchini Somalia, Fawziya Abikar amepokea dozi 200,000 za chanjo ya Sinopharm Covid 19 kutoka Nchini china.

Dozi hizo za ugonjwa wa Covid 19 zimetolewa nan chi ya china kupitia Balozi wa china nchini Somalia, Qin Jian.

Somalia ilikuwa imepokea shehena ya kwanza ya dozi 300,000 za chanjo ya ugonjwa wa Covid 19 kupitia mpango wa Covax.

Pia jumla ya watu 12,406 walithibitishwa kupatwa na maambukizi ya virusi vya corona ikiwa ni pamoja na vifo vya wagonjwa wa Covid 19 618, kulingana na takwimu kutoka wizara ya afya nchini humo.

Ugonjwa wa covid 19 unaosababisha homa kali ya mapafu inayopelekea kushindwa kupumua umesababisha vifo Zaidi ya mamilioni ya watu duniani kote na ulianzia nchini china mwishoni mwa mwaka 2019.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles