24.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Snura: Chura wangu bado ameshikiliwa

Snura Mushi
Snura Mushi

NA FESTO POLEA,

MKALI wa wimbo wa Chura, Snura Mushi ‘Majanga’ amesema  bado wimbo wake umezuiliwa licha ya kupeleka muswada mpya unaoongoza video mpya ya wimbo huo.

Snura aliwaambia waandishi wa habari visiwani hapa wakati akijiandaa na show yake ya jana usiku katika tamasha la Ziff kwamba ameshapeleka marudio ya script ya pili aliyotakiwa afanye na mamlaka husika baada ya kwanza kukataliwa.

“Wimbo wangu wa Chura bado umezuiliwa lakini kwa sasa nina wimbo mwingine unaitwa ‘Shindwe’ ukimaanisha kishindo huu utaniongezea mashabiki kutokana na kuwa katika mahadhi ya uswahilini, kisingeli,’’ alisema

Aliongeza kwamba mashabiki wa ‘Chura’ waendelee kuvuta subira hadi mamlaka husika zitakaporuhusu video hiyo kurudiwa kwa kufuata maadili yanayotakiwa.

Onyesho la jana usiku lilikuwa maalum kwa kuitwa ‘Usiku wa Bi Kidude’ ambapo wasanii na majd walioshiriki katika burudani ni wanawake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles