27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Shule za Kinondoni kunufaika na Binti Foundation

NA THERESIA GASPER

MWANAMITINDO na mbunifu wa mavazi nchini, Johar Sadiq, ameanzisha mradi maalumu unaojulikana kama Binti Foundation, ambao lengo lake ni kusaidia mahitaji mbalimbali kwa watoto wa shule za msingi nchini.

Johari alisema wameanza na wanafunzi 500 kutoka shule nne za Kinondoni ikiwemo shule ya Kumbukumbu, Mwananyamala, Msasani na Ananasifu.

“Awali tulikuwa tumelenga watoto wa kike lakini kwa sasa tumeona ni vema tusaidie kwa wanafunzi wote wakike na wakiume lengo ni kumsaidia mwanafunzi kupata mahitaji ambayo yatamuwezesha kumsaidia katika masomo yake,” alisema.

Alisema japo kwa sasa kuna mfumo wa elimu bure, lakini kuna vitu vingine wazazi hawawezi kuvimudu hivyo mradi huo utawasaidia kupata madaftari, kalamu, viatu, nguo za shule na vitu vingine mbalimbali.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles