30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

SHILOLE AWAFUNDA WASANII WA KIKE

NA SHARIFA MMASI


MSANII wa Bongo Fleva nchini, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amewataka wasanii wa kike wanaoibuka katika soko hilo kutobweteka na kutegemea mteremko ili wasonge mbele.

Shilole anayeendelea kutamba na wimbo mpya wa ‘Sitoi Kiki’, alisema muda mfupi aliokaa kimya bila kusikika, hakufulia kama inavyosemekana, badala yake aliwapa nafasi wasanii chipukizi wa kike ili nao wajitangaze sokoni.

“Kuna muda nilikaa kimya sokoni haikuwa na maana ya kwamba nilifulia kutoa ngoma mpya, badala yake niliwapa nafasi wasanii wa kike wanaoibukia sasa ili nao wajitangaze kwenye soko la Bongo Fleva.

“Binafsi bado sijaridhishwa na kazi zao, kwa sababu huwa napenda kusikiliza kazi za wenzangu kwa kuamini kwamba na wao wanazisikiliza za kwangu pia, lazima wakaze buti ili waendane na mahitaji ya soko la muziki huu,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles