31.7 C
Dar es Salaam
Thursday, March 28, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yatakiwa kuwekeza Uchumi wa Bluu

Na WINFRIDA MTOI, Mtanzania Digital

Serikali imetakiwa kuuweka  Uchumi wa Bluu(Blue Economy) katika mpango wa maendeleo kutokana na fursa nyingi za  zilizopo ikiwamo ajira. 

Kauli hiyo imetolewa na Mkufunzi wa Sheria za Kimataifa za masuala ya Bahari, Dk. Tumaini Gurumo ambaye pia ni mhadhiri wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI).

Akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wanahabari yaliyoandaliwa na Taasisi ya PS Counseling Consultants yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Dk. Tumaini, amesema kuna haja  ya Serikali kununua Meli kubwa na vifaa vingine vya uvuvi ili kufaidika na rasilimali za baharini.

Ameeleza kuwa zipo fursa nyingi lakini ukosefu wa Meli unawakosesha Wanzania ajira na kushindwa kufikia rasilimali zilizopo katika kina kirefu cha bahari.

“Kukosekana kwa meli za mafunzo ya vitendo kwa  ni kizuizi  katika kupata fursa kwa sababu inawakosesha Watanzania ajira, ni vizuri serikali ikaweka Uchumi wa Bahari katika mipango kama ilivyo kwa Uchumi wa Kijani,” amesema.

Amefafanua   kuwa Uchumi wa Bahari  unaweza kuongeza kasi ya maendeleo nchini kwa sababu kuna rasilimali nyingi zinatoka baharini ikiwamo madini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa PS Counseling Consultants, Dk. Mkumbo Mitula, amesema elimu zaidi inahitajika  kwa jamii ili kupata uelewa wa kutumia fursa za baharini.

“Uwekezaji katika uchumi wa Bluu ni muhimu lakini inahitajika elimu kuanzia ngazi za chini kama zinavyofanya nchi nyingine,” amesema Mitula.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles