31.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yataifisha madini ya bil. 1.3/-

Yisambi ShiwaJOHANES RESPICHIUS NA BARAKA MASSAWE (TSJ), DAR ES SALAAM

WAKALA wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) imekamata na kutaifisha madini yenye thamani ya Sh bilioni 1.3 yaliyokuwa yanatoroshwa kwenda nje.

Akizungumza na waandishi wa habari  Dar es Salaam jana, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari TMAA, Yisambi Shiwa, alisema  ukaguzi uliofanyika Julai 2015 hadi Januari 2016 kwenye viwanja vya ndege umewezeshwa kukamatwa  watoroshaji wa madini katika matukio 16.

“Matukio haya yalihusisha madini yenye thamani ya Sh bilioni 3.2 na kati ya hayo madini yaliyokamatwa na kutaifishwa yalipigwa mnada na kuingizia Serikali Sh bilioni 1.3

“Pia katika matukio hayo utoroshwaji huo karibu asilimia 70 ya madini hayo ni Tanzanite ikiwa asilimia kubwa yanatoka kwa wachimbaji wadogo kutokana na hali ya usimamizi katika vizimba huku Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) ukiongoza kwa utoroshwaji

“Na tangu kuanzishwa kwa ukaguzi   matukio 89 ya utoroshaji wa madini yaliripotiwa hadi Desemba mwaka jana yakiwa na thamani ya Dola za Marekani milioni 10.8 ,” alisema Shiwa.

Alisema TMAA kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imewezesha wachimbaji kuanza kulipa mapato ambako katika kipindi cha mwaka 2009 hadi Machi mwaka huu, kampuni mbalimbali zimelipa Sh  bilioni 732.6.

Wakala huyo ataendelea kusimamia na kukagua shughuuli za uzalishaji na mauzo ya madini yote nchini na   imekwisha kuweka wakaguzi katika viwanja vya ndege na mipakani   kudhibiti biashara na utoroshaji wa madini.

Naye  Giky Shamika  Kaimu Mtendaji Mkuu TMAA, alisema Wakala huyo anaangalia namna nzuri ya kuwadhibiti  watoroshaji madini wote na kubaini njia wanazopitisha.

“Kazi hii itatekelezwa kwa kushirikiana na na   Polisi, TRA, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA), Idara ya Madini na  Usalama wa Taifa  kuhakikisha inaziba mianya ya utoroshwaji wa madini mipakani na kwenye Viwanja Vya Ndege,” alisema Shamika.

Alisema  wamekuwa wakitoa elimu kwa mamlaka hizo ili kuyafahamu madini hayo iwe rahisi kuwabaini watoroshaji.

- Advertisement -
Previous article
Next article

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles