27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali yaombwa kuboresha mazingira ya uwekezaji

Na Christina Gauluhanga, Dar es Salaam

Serikali imeombwa kuzidi kuboresha mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia wawekezaji wengi wa ndani na nje hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatatu Julai 29, katika mkutano ulioandaliwa na Chama wa Waajiri Tanzania (ATE), Mkurugenzi Mtendaji, Dk. Aggrey Mlimuka amesema endapo Watanzania na wawekezaji wageni watawekeza biashara endelevu itazidi kuchagiza kwa kasi ya ukuaji wa uchumi nchini.

Amesema uwekezaji wa China ni mkubwa na wenye tija kwa Tanzania kwa sababu unaongeza ajira na viwanda hapa nchini.

“Uhusiano wa China na Tanzania ni wa muda mrefu hivyo ni vyema kuendelea kuweka Mazingira ya uwekezaji ili kuwavutia zaidi Kibiashara,”amesema Mlimuka.

Katika mkutano huo ulioandaliwa na ATE umeshirikisha wawekezaji toka nchini Norway na China.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles