26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Serikali  Uganda kuwasaidia waathirika wa maporomoko

KAMPALA, Uganda

WAZIRI Mkuu wa Uganda, Ruhakana Rugunda amesema serikali itazisaidia fedha na misaada ya chakula, familia zote zilizopoteza watu na  makazi kwenye maporomoko ya ardhi yaliyoikumba nchi hii.

Alitoa ahadi hiyo jana baada ya kuwasili  eneo la Naposho katika Wilaya ya Bududa ambalo  watu na makazi waliangamia kutokana na maporomoko ya ardhi.

Mpaka sasa Jeshi la Kulinda la Uganda (UPDF),  linaendelea kuwatoa watu walionusurika kwenye magofu ya nyumba zilizoporomoka kutokana na mvua kubwa iliyonyesha  mwishoni mwa wiki iliyopita  katika Wilaya hiyo ya Bududa, Mashariki mwa Uganda.

Inaelezwa kuwa  zaidi ya maiti 50 zimekwisha kupatikana.

Habari kutoka katika eneo lililokumbwa na  maporomoko hayo zinaeleza mpaka sasa bado mamia ya watu hawajulikani walipo huku maofisa katika wilaya hiyo  wakihofia  kuwa idadi ya waliofariki dunia  huenda ikaongezeka.

Mwandishi wa Shirika la Utanagazaji la Uingereza (BBC), aliyepo eneo alisema wakati wowote   Rais Yoweri Museveni alitarajiwa kuwasili mahali hapo  kushuhudia  maafa yaliyotokea.

Alisema madaraja  katika  mto Sume na mto Manafwa  yamevunjwa na hivyo kulazimu kuwekwa vivuko vya muda  hatua ambayo ni hatari .

Serikali imesema vikosi vya uokoaji vimefika katika eneo hilo ingawa miundombinu ya barabara na daraja lililoharibika imesababisha shughuli za uokoaji kuchukua muda mrefu.

Maporomoko mengine ya udongo yalishuhudiwa katika eneo hilo la Bududa  mwaka 2010 na yalisababisha vifo vya watu zaidi ya 300.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles