23.7 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

SERIKALI KUPANUA HUDUMA ZA MATIBABU YA DHARURA NCHINI

Na VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM

SERIKALI inakusudia kupanua huduma za matibabu ya dharura katika

Hospitali ya Kanda Mbeya na Hospitali ya Mount Meru, ili kuboresha

huduma za matibabu kwa wagonjwa wanaohitaji msaada wa dharura.

Kwa sasa hospitali pekee yenye idara maalumu inayotoa huduma ya

matibabu ya dharura nchini ni Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Hayo yalielezwa jana na Katibu Mkuu – Afya wa Wizara

ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Mpoki Ulisubsya,

alipokuwa akizindua Kongamano Kuu la

pili la Watoa Huduma za Tiba ya Dharura na Kuokoa Maisha.

“Kihistoria nchini mwetu, Hospitali ya Taifa Muhimbili ndiyo pekee ambayo ina idara maalumu kwa ajili ya kutoa huduma za dharura kwa watu wanaohitaji huduma hiyo kuokoa maisha yao,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo, Serikali imepanga kupanua wigo wa

huduma hiyo katika maeneo mengine kwa kuanzia na Hospitali ya Kanda

Mbeya na Mount Meru.

“Tunakusudia pia huduma hizi zianze kutolewa hadi katika hospitali

binafsi kisha tutaendelea hadi katika hospitali za rufaa za mikoa na

wilaya,” alisema na kuongeza:

“Kinachoendelea sasa ni kuwapa mafunzo wataalamu

ili kuongeza idadi yao, tunao 27 na hivi karibuni kuna ambao

watahitimu mafunzo na hivyo idadi hiyo itaongezeka hadi kufikia

wataalamu 36.

Alisema barani Afrika tafiti zinaonesha asilimia 40 ya watu hufariki

dunia kutokana na kucheleweshwa kufikishwa hospitalini pale

inapohitajika huduma za dharura.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Kongamano hilo, Dk. Upendo

George, alisema jumla ya wataalamu 250 wamepatiwa mafunzo kuongeza

ujuzi wao.

“Mafunzo hayo yalifanyika kabla ya kuja kwenye kongamano hili na

tumewapa mbinu ambazo wanaweza kuzitumia hata kwa kutumia vifaa

vichache walivyonavyo kuweza kuokoa maisha,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles