27.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 18, 2024

Contact us: [email protected]

SELASINI ALALAMIKA KUFINYWA MAKALIO NA KITI

Gabriel Mushi, Dodoma

Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini (Chadema) amelalamikia kufinywa makalio na kiti alichokalia bungeni leo, hatua iliyomfanya kumwomba Spika wa Bunge, Job Ndugai kuagiza ukarabati wa baadhi ya vifaa ndani ya Ukumbi wa Bunge hilo kwa kuwa asilimia kubwa ya viti vimechakaa.

Selasini ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma leo Aprili 30, wakati akiomba mwongozo kwa Spika baada ya kipindi cha maswali na majibu kumalizika.

“Mheshimiwa Spika watendaji wako wanakuangusha kwa sababu baadhi ya viti humu bungeni ni hatarishi, kwa mfano ninachokalia mimi leo kimenifinya kalio,” amesema Selasini na kusababisha wabunge na Spika kuangua vicheko.

Aidha akijibu mwongozo huo Spika Ndugai alimwambia suala hilo litachukuliwa hatua.

“Kuna watu wanauliza etu ni sehemu gani umefinywa… usijali mheshimiwa point noted,” alisema Ndugai.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles