27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

SAMIA AUNGA MKONO VITA DAWA ZA KULEVYA

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan

Na Mwandishi Wetu-MWANZA

MAKAMU wa Rais, Samia Suluhu Hassan, ameunga mkono jitihada za kupambana na dawa za kulevya, kama hatua ya kuliokoa taifa na janga hilo ambalo limesababisha madhara makubwa katika jamii.

Kauli hiyo aliitoa jana wakati akizungumza na watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, ambako alisisitiza kuwa mapambano dhidi ya dawa za kulevya yatakuwa ni endelevu lengo likiwa kukomesha uuzaji, usambazaji na utumiaji wa dawa hizo kama hatua ya kuokoa kizazi cha sasa na kijacho.

“Kamwe Serikali ya Awamu ya Tano haitarudi nyuma katika vita dhidi ya dawa za kulenya,” alisema na kuwataka wananchi waendelee kutoa taarifa za siri kwa vyombo vya dola zitakazosaidia kuwabaini watu wanaojihusisha na biashara hiyo ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles