25.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

Saidieni watoto wa kike, wajane kupata haki sawa-Wito

FRANCIS GODWIN,IRINGA

WANANCHI  wa vijiji   sita  za kata ya Image  Wilaya ya  Kilolo mkoani  Iringa,  wametakiwa  kuendelea  kuwasaidia  watoto  wa  kike na  wajane kuwa na haki  sawa ya  kumiliki ardhi na mali  nyingine katika familia  bila  kubaguliwa .

Rai   hiyo  imetolewa jana na mwezeshaji  wa asasi isiyo ya  kiserikali ya  Iringa Civil Society Organization (ICISO),  inayojihusisha na  masuala ya  elimu kwa jamii   juu ya umiliki  wa ardhi ya mali kwa  watoto  wa  kike.

Wakizungumza na  wananchi  wa  kijiji  cha Iyai, Mwezeshaji  wa  Shirika  la ICISO, Ahazi Sibale  alisema baadhi ya maeneo   kumekuwapo na ubaguzi mkubwa kwa  watoto wa  kike  kuingia katika orodha ya mgawanyo  wa mahali za familia kutokana na utamaduni wa  ovyo  kuwa  mtoto  wa  kike hapaswi  kupewa mahali kwenye familia yake  kwa  kuwa anakwenda  kuolewa .

” Wanaume  wamekuwa  wakielimishwa namna na  kuandika  wosia mapema   ili  kila mtoto kwenye familia ajue sehemu ya mali yake badala ya  kukaa  kimya na  siku  kifo  kikitokea  familia  nyuma inaanza  kunyanyasika,” alisema Sibale

Alisema  kutokana na  ubaguzi  huo,  shirika lake   kwa  kushirikiana na  kwa  kushirikiana na The Foundation for Civil Society walianza  kazi ya  kutoa  elimu kwa wananchi  wa baadhi ya  kata  za  wilaya ya  Iringa na Kilolo mkoani Iringa  ili  kupunguza ama  kumaliza ubaguzi uliokuwepo  dhidi ya watoto  wa kike kutengwa  katika  umiliki wa mahali mbali mbali .

Alisema elimu  hiyo,  imeendelea  kuwaamusha  wanawake  kuanza  kufuatilia haki  zao kwenye famili za  kupewa mgawanyo  sawa na wanaume  katika mali mbali mbali  na kwenye  ardhi na  sasa  jamii baadhi ya maeneo inawapa  haki  sawa watoto wa kiume na  wanawake katika mgawanyo wowote  wa mali za  kifamilia.

Alisema  Kata ya Image,  zaidi ya  wananchi 100  wamefikiwa na  elimu  hiyo kwa ngazi ya  kijiji na wapo  waliopewa elimu  ngazi ya kata  namna ya  kuwawezesha  wanawake  kuanzisha  vikundi   vya  kiuchumi  ili  kuondokana na  kuwa  tegemezi katika  familia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles