30.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

SAFARI YA KIPEKEE DAR- ENTEBBE NA PRECISION AIR

Mnamo tarehe 1 Julai 2017, shirika la ndege la Precision Air limezindua safari kati ya

Tanzania na Uganda na kuwapa nafasi wananchi wa nchi zote mbili kunufaika na

safari hizo kati ya Dar es Salaam-Kilimanjaro – Entebbe kwa kuongeza ufanisi katika

shughuli zao.

Nilibahatika kuwa mmoja ya abiria katika safari ya uzinduzi wa safari hizo, safari

ilianzia katika uwanja wa Julius Nyerere majira ya saa 1:10 Asubuhi,ambapo

nilijumuika na wasafiri wengine waliokuwa wakisubiri kwa shauku kubwa kuanza safari

huku wakiwa tayari na pasi zao za kusafiria pamoja na tiketi zao.

Abiria wote tulifanya utaratibu wakugonga hati zetu za safari kwa maofisa wa idara ya

uhamiaji na kuelekea katika eneo la kusubiri kuitwa kwa ajili ya kupanda ndege na

kuianza safari. Ilikua ni asubuhi nzuri, hali ya hewa ilikua ya kaubaridi huku jua

likichomoza kwa mbali. Zikisikika sauti za ngurumo za ndege zilizokuwa zikiondoka

uwanjani hapo na matangazo mabali mbali uwanjan hapo. Baada ya dakika kadhaa

nikiwa nimesimama karibu na geti namba tano nikiendelea kufurahia mandhari ya

uwanja wetu wa ndege, ilisikika sauti iliyojaa bashasha ya ukarimu ya muongoza

ratiba ya usafiri akitoa tangazo kwa abiria wote waliokuwa wakielekea Uganda

kufuata utaratibu wa kuanza kuhakiki pasi zao iliwaingie kwenye ndege tayari kuianza

safari.

Sio siri, huduma zilikuwa za kiwango cha juu kuanzia mapokezi ya abiria walipowasili

uwanjani hadi kwenye zoezi zima la kuhakiki pasi.

Mlangoni kwenye ndege alikuwa amesimama mwanadada mrembo, aliyekua amevalia

nadhifu kwenye sare za Precision Air, Huyu ni Halima Njau aliyekuwa mmoja wa

wahudumu wa Precision Air waliokuwa wenyeji wetu kwa kipindi chote cha safari

kuelekea Enteebe. Aliwakaribisha abiria wote kwa ukarimu na tabasamu la upendo

huku muhudumu mwingine wakiwapokea abiria na kuwaonyesha kila mmoja nafasi

yake.

Baada ya dakika kadhaa Rubani na muhudumu waliwaandaa abiria wote kwa tangazo

kuhakikisha kila kitu kiko sawa, na hatimaye ndege ilianza safari.

Baada ya takribani lisaa limoja ndege ilitua uwanja wa ndege wa Kilimanjaro, KIA

ambapo ndege ilikaa hapo kwa muda dakika 20 kwa ajili ya kuruhusu abiria waliokuwa

wakiishia Kilimanjaro kuteremka na kupakia wale waliokua wakienda Entebbe kutoke

a Kilimanjaro na Arusha kupanda. Wakati tukiwa uwanja wa ndege wa Kilimanjaro

niliweza kushuhudia ni jinsi gani Precision Air inautumia vyema uwanja wa

Kilimanjaro. Nilishuhudia ndege mbili zikitua katika uwanja huo, ndipo nilipo patwa

na shauku ya kutaka kujua safari za Precion Air kutoka katika uwanja huo. Baada ya

kudodosa nilielezwa ya kuwa kutokea Kilimanjaro Precision Air inasafari za kwenda

Mwanza,Zanzibar,Dar es Salaam, Nairobi na sasa Entebbe. Hili lilinifanya kutambua

mchango muhimu unaotolewa na shirika la Precision Air katika huduma ya usafari wa

anga hapa nchini.

Baada ya dakika 20 za mapumziko, tuliendelea na safari kuelekea Entebbe.

Waaoow…!! Ndivyo nilivyomskia abiria mmoja akifurahia kuuona mlima Kilimanjaro

muda mfupi baada ya ndege kuruka, Rubani alitueleza tulikua tukikatiza katikati ya

Mlima Kilimanjaro, uliokua upande wa kulia na Mlima Meru uliokua upande wa

kushoto. Niliwaona baadhi ya abiria hasa wakigeni wakifanya juhudi za kupata picha

za vivutio hivyo na hali hiyo ilinifanya nijisikie fahari kua Mtanzania. Haikuchukua

muda mrefu ambapo kabla ya Rubani hajatutaarifu tena kuwa tulikua tukikatiza kando

ya Mlima Oldanyengai ambao una volcano hai, tuliweza kushuhudia michirizi ya majivu

ikiupamba mlima huo katika kilele chake, ushahidi tosha kua volcano yake ii hai na

inatokota.

‘ona nikama mlima ule unafuka moshi…..’ alisikika mmoja wa abiria akimueleza

mwenzake. Hakika Ilikiua dhahiri ya kua kila abiria alifurahia alichokua akikiiona, na

kwa mda nilijikuta nikitamani kuwa mmoja wa wasafiri wa kila mara kuelekea

Entebbe.

Kilichotia fora zaidi katika safari nzima, ni rubani wa ndege hiyo kwa jina la Manasse

alipotuarifu abiria wote kutazama chini ili kuufurahia muonekano wa kuvutia uliokuwa

ukionekana kutoka juu.

Kwa mara ya kwanza, binafsi niliweza kuuona mlima Oldonyo Lengai kwa muonekano

kutoka angani,na kilichonifurahisha zaidi ni rubani kuahakikisha anapita katika usawa

sahihi ili abiria waweze kupata muonekano mzuri zaidi.

Safari yetu ilikua murua kabisa, na mara zote jirani yangu alikua akinileza ni jinsi gani

alikua akifurahia safari ile huku akiusifia utulivu wa ndege angani uliomfanya asinzie

mara kwa mara.

Baada ya masaa mwendo kidogo rubani alituhabarisha tena yakuwa tulikuwa tukipaa

juu ya ziwa Victoria, tuliweza kushuhudia ukubwa wa ziwa Victoria kutoka angani, na

kadri tulivyokuwa tukikaribia Entebbe tulianza kuona visiwa vichahce ziwani, na kwa

mbaali tuliweza kuona mitumbwi ya wavuvi. Hakika ilikua safari ya kipekee.

Tulipowasili katika uwanja wa ndege wa Entebbe, ndege ilitua salama. Tayari

kumbukumbu ya safari ilikua ikijirudia kichwani mwangu, picha za mandhari nzuri

nilizo ziona toka mwanzo wa safari zilikua zikijirudia kichwani mwangu. Matone ya

maji kwenye dirisha yana nirudisha kwenye wakati halisi, hii haikua mvua bali ni

salamau maalumu ya kutukaribisha rasmi katika uwanja wa ndege wa Entebbe, salamu

hii hutolewa kwamagari mawili ya zima moto kurusha maji hewani huku yakitazamana

na ndege hukatiza katikati. Ishara hii ili ashiria kuanza rasmi kwa safari za Precision

Air nchini Uganda.

Wahudumu pamoja na rubani walitutakia abiria wote kheri kabla ya kushukuru na

tiliposhuka chini tulikaribishwa na wahudumu wengine wa Precision Air kwa furaha.

Safari hili kwangu binafsi imekuwa ya aina yake kupaa na Precision Air, na sita sita

kumshawishi mtu yeyote kusafiri na Precision Air, kwani nna uhakika hata yeye

ataifurahia.

Nikiwa naandika haya yote, naendelea kutafakari ni jinsi gani Tnazania na Uganda

watanufaika na safari hizi za Precision Air. Tayari nawaona wafanyakazi wa Jumuiya

yetu ya Afrika mashariki wakitumia safari hizi katika kuongeza ufanisi katika utendaji

wao kwa zile shughuli zinazo wahitaji kusafiri. Nawaona pia wafanyakazi wa mradi wa

bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Tanga nchini Tanzania wakiitumia Precision Air

katika kufanikisha shughuli zao za kiutendaji. Wakati huo huo nawaona wananchi wa

Uganda wakitumia fursa ya safari hizi kufanya utalii kwa vivutio kama Zanzibar na

Serengeti.

Nawaona pia wafanyabiashara wa mavazi na urembo kutoka Tanzania

wanavyochangamkia safari hizi katika kuongeza tija katika biashara zao.

Binafsi niseme asanteni Precision Air kwa fursa hii, kwani kupitia mtandao wenu wa

safari zenu mmeendelea kuifungua Tanzania. Naisubiri kwa hamu ile siku ntapata

fursa ya kusafiri na nyinyi tena.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles