23 C
Dar es Salaam
Saturday, April 20, 2024

Contact us: [email protected]

Saccos zatakiwa kuwekeza kwenye viwanda

Upendo Fundisha, Mbeya

Serikali imevitaka Vyama vya Ushirika na Vyama wa Akiba na Mikopo (Saccos) nchini kuwekeza kwenye viwanda vikubwa  ili kukuza uchumi wao na nchi kwa ujumla.

Hayo yameelezwa leo na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Ntinika wakati akizindua maonyesho ya maadhimisho ya vyama vya ushirika duniani ambapo kitaifa yanafanyika mkoani Mbeya.

“Viwanda hivyo vitasaidia kubadilisha mfumo wa maisha ya wazalishaji kwani bidhaa nyingi za mazao zitakidhi viwango vya ubora na kukamata soko la kimataifa,” amesema Ntinika ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Albert Chalamila.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Paul Ntinika (wa pili kulia), akipata maelekezo ya uzalishaji wa samaki kutoka kwa mwakilishi wa Chama cha Ushirika cha Kahama. PICHA NA UPENDO FUNDISHA

Naye Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Ushirika nchini, Theresia Chitumbi, amesema vyama hivyo vinakabiliwa na changamoto ya elimu ya fedha hivyo kushindwa kufikia malengo.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa Chama cha Ushirika cha Kahama Cooperative Union, Emmanuel Charahani, ameiomba Serikali kuwasaidia kutafuta masoko ya bidhaa zao kwani uwezo wa kuanzisha viwanda wanao kulingana na mitaji wanayoimiliki kuwa zaidi ya Sh bilioni 30.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles