33.2 C
Dar es Salaam
Friday, March 29, 2024

Contact us: [email protected]

RUGE MUTAHABA AMEZIKWA KISHUJAA KIJIJINI KWAO KIZIRI, BUKOKA

Elizabeth Joachim -Dar es salaam.

Aliyekuwa mkurugenzi wa vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amezikwa kishujaa na idadi kubwa ya watu wakiwemo viongozi wa serikali ngazi mbalimbali, wasanii, taasisis binafsi na watu wenye vipawa tofauti kutoka ndani ya mkoa wa Kagera na nje ya mkoa huo.

Mazishi hayo yamefanyika leo Machi 4 huko kijijini kwao Kiziru, Bukoba huku mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group Joseph Kusaga akiahidi kuendeleza mazuri yaliyoachwa na Ruge Mutahaba.

Ameyasema hayo katika viwanja vya Gymkhana Bukoba wakati wakiaga mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba na kisha kupumzishwa katika makao yake ya milele katika makaburi ya familia yaliyopo karibu na nyumba ya baba yake.

“Ruge alikuwa kinara wa mambo mengi mazuri alikuwa na talanta kubwa ya utunzi wa vipindi mbalimbali, Malkia wa nguvu, Kipepeo pamoja na Fursa ni baadhi ya vitu tutakavyo vienzi na kuviendeleza,” amesema Kusaga.

Mutahaba amefariki dunia Februari 26 Mwaka huu nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kusumbuliwa na figo kwa muda. Ameacha watoto watano wanne wa kiume na mmoja wa Kike.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
585,000SubscribersSubscribe

Latest Articles