25.2 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

RUBY ADAI HANA UKARIBU NA ALI KIBA

Na JOHANES RESPICHIUS

BAADA ya habari kusambaa kwenye mitandao ya kijamii zikihoji ukaribu unaohusishwa na kutoka kimapenzi baina ya waimbaji nyota wa Bongo Fleva, Hellen George ‘Ruby’ na Ali Kiba, mrembo huyo amesema hana ukaribu wowote na msanii huyo.

Ruby anayefanya poa na ngoma yake ‘Walewale’ amelipasha Swaggaz kuwa taarifa za ukaribu wake na Kiba amekuwa akiziona kwenye mitandao ya kijamii lakini hakuna kinachoendelea kati yao kwani hata namba yake ya simu hajawahi kuwa nayo.

“Na mimi taarifa hizo nimekuwa nikiziona kama wewe ulivyoziona, sioni jipya kwasababu walishawahi kusema kuwa nipo karibu sana na Diamond, sasa wamegeukia kwa Kiba ambaye hata mawasiliano yake sijawahi kuwa nayo,” alisema Ruby.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles