27.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 23, 2024

Contact us: [email protected]

RPC DAR, IRINGA WAGONGANA MWANAFUNZI ALIYETOWEKA, WAFAFANUA

WAANDISHI WETU DAR, IRINGA


KAULI za makamanda wa polisi, Lazaro Mambosasa wa Kanda Maalumu Dar es Salaam na Juma Bwire wa Iringa kuhusu kutoweka kwa Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Abdul  Nondo (24), zimezua utata baada ya kukinzana.

Wakati Kamanda Mambosasa akisema Nondo alikamatwa akiwa Mafinga akiendelea na shughuli zake, Kamanda Bwire alieleza awali kuwa mwanafunzi huyo aliripoti polisi Mafinga.

Machi 8, baada ya Nondo kupatikana,  Kamanda Bwire alizungumza na waandishi wa habari akaeleza kuwa ni mwanafunzi wa  mwaka wa tatu, kitivo cha siasa na utalawa katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye inasemekana alipotea katika mazingira ya kutatanisha mkoani Dar es Salaam.

“Jana tarehe saba, mwezi wa tatu, majira ya saa moja alifika katika Kituo cha Polisi cha Mafinga, |Wilaya ya Mufindi na kueleza kuwa  ametekwa na watu wasiofahamika,” aikaririwa akieleza Kamanda Bwire.

Baada ya kuhojiwa mkoani Iringa, Nondo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), alisafirishwa kuletwa Dar es Salaam.

Juzi, Kamanda Mambosasa alizungumza na waandishi wa habari akaeleza kuwa ili kuthibitisha kile kilichokuwa kimezagaa  kuwa ametekwa na watu wasiojulikana, hakuripoti mahali popote, si kwa mwenyekiti wa mtaa, si kwa afisa mtendaji wa kata wala kituo chochote cha polisi mkoani Iringa, alikamatawa akiwa Mafinga akiendelea na shughuli zake za kawaida.

Wafafanua kauli zao

Kutokana na kauli hizo, gazeti hili liliwatafuta makamanda hao ili kufafanua kauli zao.

Kamanda Bwire alisema suala la Nondo kwa sasa linachunguzwa na Jeshi la Polisi, Dar es Salaam hivyo hawezi  kulizungumzia.

Kwa upande wake Kamanda Mambosasa alisema kwa kawaida upelelezi hauwezi kuwekwa hadharani, bali kinachotolewa ni matokeo ya upelelezi huo.

“Hayo ni matokeo ya upelelezi kwa hiyo uchunguzi umeonyesha hivyo, tena ni uchunguzi wa kisayansi.

“Yani utekwe usinyang’anywe simu kisha uachiwe bila kuripoti popote uendelee na kazi zako,” alisema Kamanda Mambosasa.

Kwa habari zaidi jipatie nakala ya gazeti la MTANZANIA.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles