23.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 19, 2024

Contact us: [email protected]

ROSE NDAUKA: WANAUME WAKWARE BADO WANANISUMBUA

Na JESSCA NANGAWE


STAA wa filamu nchini, Rose Ndauka, ameweka wazi kwamba licha ya kujibidisha kwenye ubunifu wa kazi mbalimbali za kumwingizia kipato anazozifanya, hujikuta akikutana na idadi kubwa ya wanaume wakware wanaomtaka kimapenzi badala ya kufanya naye biashara.

Ndauka ambaye kwa sasa anajishughulisha na ujasiriamali, alisema amekua akibuni njia mbalimbali za kumwingizia kipato ili aendane na hali halisi ya maisha kwa sasa lakini wanaume wakware humkwamisha kwa usumbufu juu yake.

“Kila kazi ina changamoto zake, sikatai wanaume lakini wengi wao huja kunitaka kimapenzi, badala ya kuzungumzia masuala mengine ya biashara, nachukizwa sana na wanaume wa aina hii,” alieleza Ndauka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles